
Jinsi ya Kuomba AVN NACTVET Award Verification Number (AVN) Haya ni maelezo kuhusu uthibitisho wa vyeti na utaratibu wa kujiunga kwa wanafunzi waliomaliza stashahada kutoka vyuo vinavyotambuliwa na NACTE au TCU
Uthibitisho wa Cheti (Award Verification Number – AVN)
Ili kupata namba ya uthibitisho wa cheti (AVN), mwanafunzi lazima awe amehitimu Stashahada (Diploma) kutoka chuo kinachotambulika na:
- NACTE (Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi) au
- TCU (Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania)
Masharti na Utaratibu wa Kuomba
Kwa wanafunzi waliomaliza Stashahada
- Mwaka 1961 hadi 2014:
- Wapakie cheti cha Diploma pamoja na nakala ya matokeo (Transcript) kwa mfumo wa PDF.
- Walio na Cheti cha Ufundi Kamili (FTC) kutoka NECTA:
- Wanaweza kutumia namba yao ya mwisho ya mtihani kama ilivyo kwenye cheti. Mfano:
U0000/0000/0000
.
- Wanaweza kutumia namba yao ya mwisho ya mtihani kama ilivyo kwenye cheti. Mfano:
- Waliomaliza kuanzia 2015 hadi sasa:
- Lazima wawe na matokeo yanayotambulika na chuo na yaliyopo kwenye mfumo wa NACTE.
- Format ya namba inaweza kuwa:
NSXXXX/XXXX/XXXX
NPXXX/XXXX/XXXX
- Au nyingine yoyote iliyosajiliwa chuoni (Wasiliana na Afisa wa Udahili wa chuo husika).
Vigezo vya Elimu ya Sekondari
- Wote wanatakiwa kuwa na Cheti cha Elimu ya Sekondari (CSEE)
- Na angalau pass nne (4) katika masomo yasiyo ya kidini.
- Waliomaliza CSEE kabla ya 1988, au Walimu kabla ya 2010, au wenye vyeti vya kabla ya 2015:
- Wapakie vyeti na transcript zao za masomo.
Wenye Vyeti vya Kigeni
- Wenye elimu ya sekondari kutoka nje ya Tanzania:
- Lazima waombe usawa wa vyeti kutoka NECTA.
- Wenye stashahada kutoka nje ya nchi:
- Wapate usawa wa vyeti kutoka NACTE.
Jinsi ya Kuhakiki Taarifa za Mwanafunzi kwa Ajili ya AVN
Hatua | Maelezo |
---|---|
1 | Tembelea tovuti ya NACTE https://www.nactvet.go.tz |
2 | Bofya “Students Information Verification” |
3 | Weka namba ya mtihani wa CSEE au namba ya usajili wa Diploma |
4 | Kama umesahau nenosiri (password), bofya “Forgot Password” |
5 | Ingiza jina la mtumiaji, namba ya simu au barua pepe uliyotumia kusajili |
6 | Mfumo utatuma nenosiri jipya kwenye namba ya simu na barua pepe yako |
Kwa Wahitimu Kutoka Vyuo Hivi
Wanafunzi waliomaliza kutoka vyuo vifuatavyo wanapaswa kuhakikisha taarifa zao zipo kwenye mfumo wa NACTE:
- Dar es Salaam Institute of Technology (DIT)
- Mbeya University of Science and Technology (MUST)
- Arusha Technical College (ATC)
- Karume Institute of Science and Technology (KIST)