Hili hapa tangazo la Nafasi za Kazi Conservation Ranger III – Boat Operator Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Mwombaji anatakiwa awe na Cheti cha Kidato cha Nne (Form Four) pamoja na Cheti katika mojawapo ya fani zifuatazo: Usafirishaji wa Majini (Maritime Transport), Uhandisi wa Meli (Marine Engineering), Usimamizi wa Usafirishaji na Mizigo (Shipping and Logistics Management), au sifa nyingine zinazofanana kutoka taasisi inayotambulika.

Mwombaji pia anatakiwa awe na Cheti cha Lazima (Mandatory Certificate) cha uendeshaji wa vivuko kilichoidhinishwa na Chuo cha Dar es Salaam Maritime Institute au taasisi nyingine inayotambulika na Serikali/IMO, pamoja na cheti cha Rating Forming Part of Navigation Watch kilichotolewa na TASAC au taasisi nyingine inayotambulika na Serikali/IMO, na awe amehudhuria mafunzo ya angalau miezi sita (6) baharini katika huduma za Meli/Majini.
Pia, mwombaji atatakiwa kuhudhuria na kufaulu mafunzo ya awali ya kijeshi (recruit).
Tuma maombi hapa https://portal.ajira.go.tz/advert/display_advert/10414