Hili hapa tangazo la Nafasi za Kazi Director of Licensing Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Mwombaji anatakiwa awe na Shahada ya Uzamili (Master) katika mojawapo ya fani hizi: Uchumi, Sheria, Uchumi wa Kilimo, Biashara ya Kilimo, Takwimu, Biashara ya Kimataifa, Uchumi na Fedha, Masoko, Ujasiriamali, Usimamizi wa Biashara au fani nyingine inayofanana kutoka taasisi ya elimu ya juu inayotambulika. Shahada ya Uzamili hiyo inatakiwa iendane na Shahada ya Kwanza (Bachelor).

Pia, mwombaji anatakiwa awe na uzoefu wa kazi wa angalau miaka KUMI (10) katika fani zinazohusiana, ambapo kati ya hiyo, angalau miaka MIWILI (2) iwe katika nafasi ya uongozi.
Tuma maombi hapa https://portal.ajira.go.tz/advert/display_advert/10427