Nafasi za Kazi Wilaya ya Songea 30 May 2025 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea amepokea kibali cha Ajira chenye Kumb. Na. FA.97/288/01/A/25 cha tarehe 29/04/2025 kutoka kwa katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea anatangaza nafasi za kazi na anakaribisha maombi kwa Watanzania wote wenye sifa za kujaza nafasi hizo kama ifuatavyo:-

Ajira mpya zilizotangazwa
1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 5
- Kuajiriwa Wahitimu wa Kidato cha Nne (Form Four) wenye Stashahada (Diploma) ya Uhazili au cheti cha NTA level 6 ya Uhazili. Aidha, wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kingereza maneno 100 kwa dakika moja na kupata mafunzo ya programu za kompyuta za ofisi kama vile: Word, Excel, Powepoint, Internet, E-mail na Publisher kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
2. Dereva Daraja II – Nafasi 3
- Mwombaji awe amehitimu Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV), au Sita (VI), awe na Leseni ya Daraja C au E ya uendeshaji magari ambayo amefanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja bila kusababisha ajali. Awe amehudhuria mafunzo ya msingi ya uendeshaji magari (Basic Driving course) yanayotolewa na chuo cha VETA au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
Jinsi ya kutuma maombi
Barua ziandikwe kwa Anwani ifuatayo;- Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), Halmashauri ya Wilaya ya Songea, 1barabara ya Halmashauri, S. L. P 995, 57183 SONGEA, RUVUMА.
Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo; https://portal.ajira.go.tz (Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sektretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa (‘Recruitment Portal’).