Hii hapa orodha ya majina ya walioitwa kazini Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinapenda kuwataarifu waombaji kazi mbalimbali waliofanya usaili tarehe 15 hadi 17 Mei, 2025 kuwa, majina ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyo orodheshwa katika tangazo hili.

Waombaji waliofaulu usaili watatakiwa kukamilisha taratibu mbalimbali za ajira kwa kufika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jengo la Utawala, Ofisi ya Masjala, Chumba Na. 315 siku ya Jumatatu, tarehe 2 Juni, 2025 kuanzia saa tatu kamili asubuhi, wakiwa na nyaraka zilizoainishwa katika tangazo hili ili ziweze kuhakikiwa kabla ya kupewa barua za ajira.
Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili, watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa.
Nyaraka za kuwasilisha ni kama ifuatavyo
- Vyeti halisi (Original Certificates and Transcripts) na nakala mbili za vyeti hivyo ambazo zimethibitishwa na Mamlaka za kisheria ( certified by Advocate/Magistrate) vya masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea;
- Cheti cha kuzaliwa;
- Nakala ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA); na
- Picha ndogo nne za rangi (four coloured passport size photographs)